Sehemu ya Kwanza
Lengo Kuu: Kujua mapepo na kazi zake.
Lengo Mahsusi: Kujua namna ya kuzishinda roho za kipepo na kazi zake.
MAPEPO
Ni roho chafu, roho za mashetani, ziwaingiazo watu ili kuwatesa kwa magonjwa na mateso anuwai.
“Naye Yesu akisha kuona kuwa mkutano unakusanyika mbio, akamkemea yule
pepo mchafu akamwambia, Ewe pepo bubu na kiziwi,mimi nakuamuru mtoke
huyu, wala usimwingie tena”(Marko 9:25) pia (Mt 4:24 &7:22).
Sifa kuu ya Mapepo ni kuwa, hayana umbo, nyama wala mifupa. Ni roho, na
roho haiwezi kuwa na mwili wala mifupa (Luka 24:39)”....ni
shikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili wala mifupa...”
Isipokuwa, Huweza kuingia ndani ya mwili wa kiumbe hai na kuvaa umbo na
sura yake.
Kumbuka: Hii ziyo mizimu au Roho za wafu. Mtu
akishakufa, roho yake haina uwezo wa kurudi duniani. Usidanganyike.
Fuatilia kisa cha tajiri na masikini, roho ya tajiri haikuweza kurudi
duniani. (Luka 16:27-31)
Wala, roho hizi(mapepo) siyo malaika
walioasi, kwa kuwa wao wametekwa na tayali wako kwenye kamaba zao
wakingoja siku ya hukumu (Yuda 1:16,2Petro 2:4)
Swali: Je, mkuu wa mapepo ni nani? Ili kupata jibu fuatana nami.....
Biblia katika kitabu cha Marko 3:22, imeeleza wazi, aliye mkuu wa
mapepo. Naye ni Beelzebuli. Hili ni dhahili, kuwa huyu ndiye mkuu wa
mapepo na ndiye pepo mkuu.
Je, mapepo yanamfahamu Mungu, yanamchukuliaje?
Mepepo yanafahamu fika kuwa Mungu yupo. Tena yanajua kuwa Mungu
anauwezo na nguvu zaidi yao, ndiyo maana humwogopa. (Yakobo 2:19).”Wewe
waamuni ya kuwa Mungu ni mmoja; watenad vema.mashetani nao wanaamini na
kutetemeka”
Kama vile mapepo yanavyomogopa Mungu na hata
kutetemeka, kadharika mtu asiye na roho wa Mungu, huyaogopa mapepo. Je,
hujaona mtu anaogopa kulala peke yake ndani, pengine hata mchana huogopa
kubaki nyumbani peke yake wengine wanapokuwa hawapo? Hata wanafunzi wa
Yesu, kabla ya kumpokea Roho Mtakatifu, walikuwa waoga juu ya pepo.
(Mathayo 14:26,Luka 24:37). Hivyo, watu wote, wanapaswa kuokoka na
kupokea nguvu ya Roho mtakatifu ili kuwashinda mapepo na kazi zao zote.
Zingatia hili, mapepo yananao uwezo wa kutenda miujiza kupitia watu,
vitu na hata wanayama ili kuwadanganya watu na miujiza yao ya uongo
(Ufunuo 16:14).
Hakika, kazi za mapepo zikidhibitiwa vilivyo, kazi
zote za adui/ shetani zitakuwa zimeshindwa na maangamizi yote ya kipepo
hayatapata nafasi tena. Amen.
Je, kuna uhusiano gani kati ya watu/ binadamu na mapepo? Chanzo/asili yake ni nini? Endelea kufuatana nami toleo lijilo.......
Mwl. Sospeter Simon S. Ndabagoye
New Elshaddai Ministries NEM-Tanzania.
+255 757 464 141
+255 784 464 141
+255 712 909 021.
E-mail sos.sesi@yahoo.com.
Mungu Awabariki Sana.
No comments:
Post a Comment