Translate

Saturday, August 24, 2013

KUDUMU KATIKA MAOMBI



Bwana Yesu asifiwe sana.

Namshukuru Mungu kwaajili yako unaesoma ujembe huu-Mungu akubariki sana na kukuepusha na balaa zote,afute laana na mikosi inayokuzunguka katika jina la Yesu Kristo.

Ndugu yangu, naomba nikukaribishe katika somo letu la leo:

 MADA KUU: KUDUMU KATIKA MAOMBI.

Kwanza Kabisa,naomba kukueleza kwaufupi sana kuwa Dhana ya  "kuomba" ni kuwasilisha mahitaji ili upatiwe msaada.
Aidha, kwa muktadha huu, kuomba ni kuwasiliana na Mungu ambaye ndiye baba yetu na mwokozi wa maisha yetu-Haleluya!

(A)Maandalizi kabla ya kuanza Kuomba.

(i) Hakikisha Moyo wako ni safi mbele za Mungu, usiwe na kinyongo,hasira wala mwenye mawazo mabaya, hivyo jitakase kwanza kabla ya kuanza maombi.Zaburi  29:2b...mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu
(ii) Tubu ili utakaswe hata Mungu akusikilize,omba rehema za Mungu ziwe juu yako ndipo uanze kuomba Isaya 1:18.

(B)Namna ya kuomba.

(i) Kwanza maombi ni lazima ujue unaomba nini na kwa nani.
Yesu alisema, na lolote mtakaloomba kwa Baba yangu, ombeni kwa jina Langu,tena akasema, na lolote mtakaloomba kwa jina langu, mmeshapata.
Hivyo, yakupasa kuomba kwa usahihi,kupitia Jina la Yesu kwa kuwa ndilo jina pekee tulilopewa wanadamu kuolewa kwalo....na zaidi hili ndilo jina kuu kuliko majina yote Wafilipi 2:10-11
Maana yake ni kuwa,kuomba kwa kupitia jina lingine ni sawa na kukosea namba za unaempigia simu,je unataegemea kumpata unayempigia simu?
Kwa ufupi. usalipo usizunguke,piga moja kwa moja kwa Yesu naye atatenda hapo hapo.
(ii) Jenga Imani  ya kuwa Mungu hashindwi wala si kigeugeu,kila uombacho sharti upate kwa mapenzi yake. Mathayo 7:7,tena kuwa thabiti katika maombi yako hata kwa kufunga Mathayo 17:20-21.
(iii) Kuwa na msatari wa kusimamia katika maombi yako,kwa kuwa Bwana anasema leteni hoja zenye nguvu, tena anaongeza "unikumbushe na tuhojiane....Isaya 43:26,BWANA anakuona na yuko tayari kukuhudumia endapo utachukua hatua ya kuomba kwa imani Yeremia  29:11-12
(iv) Kuwa tayari kwa matokeo yoyote ilimradi yameamriwa na Mungu yatokee,Shukuruni kwa kila jambo,na kila jambo na wakati wake,usilazimishe Mungu afanye vile unataka,yaache yaliyomapenzi yake yatimie Mathayo 7:10,pia Muhubiri 3:1.

(C)Mwisho wa Maombi.
Hitimisha kwa kushangilia kwa kuwa Mungu ameyasikia maombi yako na yuko tayari kufanya vile anavyoona inafaa.

Jitakase tena,omba ulinzi wa Roho mtakatifu,soma biblia,endelea kukua katika hali ya kumpenda Mungu na Utamani zaidi kujifunza mengi kutoka kwake.Mungu akubariki,akuinue na ukupe muujiza wake katika jina la Yesu Kristo.

Amen

No comments:

Post a Comment